Proverbs 6:20-25

Onyo Dhidi Ya Uasherati


20 aMwanangu, zishike amri za baba yako,
wala usiyaache mafundisho ya mama yako.

21 bYafunge katika moyo wako daima,
yakaze kuizunguka shingo yako.

22 cWakati utembeapo, yatakuongoza;
wakati ulalapo, yatakulinda;
wakati uamkapo, yatazungumza nawe.

23 dKwa maana amri hizi ni taa,
mafundisho haya ni mwanga
na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,

24 eyakikulinda na mwanamke aliyepotoka,
kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.

25 fMoyo wako usitamani uzuri wake
wala macho yake yasikuteke,
Copyright information for SwhKC